Klabu ya West Ham United yenye maskani yake London imeonesha nia ya kumsajili aliyekuwa kiungo wa Chelsea, N’Golo Kante ambaye alitimkia Uarabuni mnamo 2023 baada ya miaka 7 ya uhudumu wake kunako klabu ya Chelsea.
Klabu ya West Ham United yenye maskani yake London imeonesha nia ya kumsajili aliyekuwa kiungo wa Chelsea, N’Golo Kante ambaye alitimkia Uarabuni mnamo 2023 baada ya miaka 7 ya uhudumu wake kunako klabu ya Chelsea. Kante (33) raia wa Ufaransa ambaye kwa sasa anachezea Al Ittihad ya Saudi Arabia huenda akarejea London ikiwa Wagonga nyundo hao watapeleka dau ambalo linatajwa kugharimu pauni milioni 20 ingawa mshahara wa nyota huyo wa zamani wa Leicester City ukitajwa kuwa kikwazo.