Tue, 27 Feb 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Samuel Eto'o alipewa uhuru wa maamuzi kwenye uendeshaji wa Shirikisho la soka nchini Cameroon na vitu vingine lakini yamekuwa majanga ndio maana serikali ikaingilia kati kuweka mambo sawa.
Ofisi wa Waziri mkuu imepokea maagizo ya kuunda kamati kutoka kwa Rais ili ifanye uchunguzi wa kujua nini tatizo na namna bora ya kutatua changamoto hizo.
Kamati hiyo imeundwa na watu kutoka ofisi ya Waziri mkuu, Ofisi ya Rais, na wizara ya michezo lakini Rais wa Shirikisho hilo Samuel Eto'o si sehemu ya kamati hiyo.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live