Mon, 19 Dec 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Historia inatuonyesha kuwa Ronaldinho Gaucho, Kylian Mbappe na Lionel Messi wametwaa taji la Kombe la Dunia mwaka mmoja tu baada ya kujiunga na klabu ya Paris Saint-Germain.
Mwaka 2001 Ronaldinho anatua PSG akitokea klabu ya Gremio na mwaka 2002 anatwaa World Cup na Brazil.
Mwaka 2017 Kylian Mbappe anajiunga na PSG akitokea klabu ya Monaco na mwaka 2018 ananyanyua ndoo na Ufaransa.
Mwaka 2021 Lionel Messi anatua PSG akitokea Barcelona na hatimaye 2022 anashinda Kombe la Dunia na wababe Argentina.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live