Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa Bodi ya Ligi (TPLB) Karim Boimanda amesema kama shabiki hajanunua tiketi na hana mualiko asiende uwanjani akitegemea kuingia bure.
Karim amesema kuwa hata vitambulisho vya msimu huu havitatumika katika huo mchezo wa Yanga SC na Simba SC utakaochezwa Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam.
“Kwa wale wageni wanaoalikwa kutazama mchezo huo watapatiwa kadi maalumu ambayo huwezi kumpa mtu mwingine atumie, eneo la VVIP watakaa watu maalumu ambao wamealikwa tu.
“Wengine kama hauna kinachokufanya uingie kiwanjani ni bora usije maana hautaingia uwanjani kwenyewe na watoto tunawapenda lakini siku hiyo wataruhusiwa wale wenye kadi tu,“ alisema Karim.