Kocha wa zamani wa timu ya Taifa ya Ubelgiji, Marc Wilmots yupo ukingoni kutangazwa kama kocha mkuu wa klabu ya Kaizer Chiefs ya Afrika Kusini baada ya pande zote kufikia makubaliano.
Kocha wa zamani wa timu ya Taifa ya Ubelgiji, Marc Wilmots yupo ukingoni kutangazwa kama kocha mkuu wa klabu ya Kaizer Chiefs ya Afrika Kusini baada ya pande zote kufikia makubaliano. Wilmots (54) ambaye amewahi kuinoa Raja Casablanca, timu za Taifa za Ivory Coast na Iran anatarajiwa kumwaga wino kwa mkataba wa miaka mitatu huku akitia kibindoni mshahara unaotajwa kuwa Randi 104,000 (Tsh milioni 14) kwa mwezi.