Wed, 5 Jun 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mshambuliaji wa Arsenal, Kai Havertz amedai kuwa kuhama kutoka Chelsea kwenda Arsenal lilikuwa jambo kubwa sana.
"Mashabiki wa Chelsea walikasirika sana nilipoondoka, mashabiki wa Arsenal nao hawakufurahia nilipofika sababu mwanzo wangu haukuwa mzuri."
"Lakini uwepo wa kocha mwenye nguvu, wachezaji wenzangu wenye nguvu ambao muda wote wanakupa ushirikiano linakuwa jambo kubwa. Kuhama kutoka Chelsea kwenda Arsenal lilikuwa jambo kubwa sana," amesema Kai Havertz.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live