Tue, 30 Jul 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kiungo mpya mkabaji wa Simba, Yusuph Kagoma (28) atakaa nje ya uwanja kwa wiki mbili hadi tatu baada ya kupata majeraha akiwa kambini Ismailia, Misri.
Kagoma ni kati ya wachezaji ambao wamesajiliwa na Simba katika dirisha kubwa la usajili akitokea Singida Fountain Gate katika msiu uliopita.
Hadi hivi sasa bado taarifa rasmi haijatolewa majeraha ambayo ameyapata akiwa kambini huko wakijiandaa na msimu ujao, hivyo kiungo huyo atakosekana katika Kariakoo Dabi itakayopigwa Agosti 8, mwaka huu kwenye Uwanja wa Mkapa, Dar.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live