Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Kagera yaipeleka Yanga Mwanza

Yanga Above Kikosi cha Yanga

Thu, 10 Nov 2022 Chanzo: Mwanaspoti

Baada ya kuthibitishwa mchezo wa Kagera Sugar na Yanga kupigwa Uwanja wa CCM Kirumba jijini hapa, Kagera Sugar wameeleza sababu za kuuhamisha mchezo huo kutoka Kaitaba huku ukilia na kasi ndogo ya ukarabati wa Uwanja wa Kaitaba licha ya kusaidia zoezi hilo kwa fedha.

Mchezo huo wa raundi ya 11 utachezwa Novemba 13 utakuwa wa tano wa nyumbani kwa Kagera Sugar kwenye uwanja huo huku mmoja pekee ukipigwa Kaitaba dhidi ya Singida Big Stars ambao ilicheza bila mashabiki.

Katibu wa Kagera Sugar, Ally Masoud, alisema sababu kubwa ya kupeleka mchezo huo Mwanza ni kutokukamilika kwa uwanja wao huku kikosi kikijifua mjini Bukoba kwa maandalizi ya mchezo huo.Katibu wa Chama cha Soka mkoa wa Kagera (KRFA), Al-amin Abdul alisema wamefuatilia matumizi ya fedha hizo na utekelezaji wa mradi lakini manispaa imekuwa ikitoa majibu yasiyoeleweka ambapo amejivua lawama na kuwatupia zigo hilo.

Akitolea ufafanuzi wa madai hayo, Afisa Michezo na Utamaduni Manispaa ya Bukoba, Cletus Mutakyawa, alikiri Kagera Sugar kutoa fedha kwa ajili ya kuharakisha uwekaji wa uzio ambao uliondolewa wakati wa sherehe za kuzima Mwenge wa Uhuru Oktoba 14 mwaka huu.

Alisema fedha hizo (akigoma kutaja kiasi) ziliwekwa na Kagera Sugar kwa makubaliano maalum na Manispaa ya Bukoba kuwa baadae zitarejeshwa kwani ilikuwa ni dharura kuharakisha ukarabati huo huku akisisitiza kuwa matumizi ya fedha hizo lazima yafuate taratibu za Serikali.

Hata hivyo alieleza kuwa ujenzi wa uzio huo umeshakamilika siku tatu zilizopita na tayari Bodi ya Ligi imejulishwa.

“Wao wakati wanapiga kelele sisi tayari tulikuwa tumeanza kazi na uzio umekamilika tangu juzi na tumewatumia picha. Ni kweli fedha zilitolewa na Kagera Sugar lakini zitarudishwa.”

Chanzo: Mwanaspoti