Sun, 3 Mar 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Wenyeji, Kagera Sugar wamelazimishwa sare ya kufungana bao 1-1 na JKT Tanzania katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara jana Jumamosi Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba.
JKT Tanzania walitangulia na bao la Edward Songo dakika ya 22, kabla ya Mubarak Hamza kuisawazishia Kagera Sugar kwa penalti dakika ya 41.
Kwa matokeo hayo, Kagera Sugar inafikisha pointi 23 katika mchezo wa 19, ingawa inabaki nafasi ya saba na JKT Tanzania inafikisha pointi 19 katika mchezo wa 18 ingawa inabaki nafasi ya 12.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live