Mon, 29 Jan 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Wekundu wa Msimbazi Simba SC, wanarejea Ligi Kuu ya NBC kwa kuanza kucheza mechi zao za viporo ambapo wataanza na Mashujaa FC katika Uwanja wa Lake Tanganyika Februari 3, 2024.
Baada ya kumalizana na Mashujaa, Simba atasafiri hadi Tabora katika Uwanja wa Ali Hassani Mwinyi kuwafuata Tabora United Februari 6 na kisha watarejea nyumbani kuwakaribisha Azam FC Februari 9 ambapo uwanja watakaochezea utatangazwa baadae.
Baada ya Azam FC, Simba wataelekea jijini Mwanza kuwakabili Geita Gold katika dimba la CCM Kirumba Februari 12,2024.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live