Straika wa zamani wa Vilabu vya Ajax, Juventus, Inter Milan, AC Milan, Man United, PSG, Barcelona, LA Galaxy na Timu ya Taifa ya Sweden Zlatan Ibrahimovic ametupa kisa kinachoonesha muendelezo wa ubabe wake katika soka.
Akizungumza Zlatan anasema
"Nilikuwa Juventus, na tulicheza dhidi ya Inter. Materazzi alinikabili na niliumia. Miaka minne baadaye nilimpiga teke, Nilimpeleka hospitali. Dejan Stankovic aliniuliza 'Kwa nini ulifanya hivyo?' Nilimwambia: 'Nimekuwa nikingojea hii kwa miaka 4."
Zlatan ametangaza kustaafu Soka la kiushindani mwaka huu (2023) baada ya kudumu kwa miongo takribani miwili.