Mon, 3 Jul 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
KMC iko kwenye mazungumzo ya kumpata kiungo wa Namungo, Lucas Kikoti ili akaichezee timu hiyo msimu ujao.
Kocha wa KMC, Jamhuri Kihwelo Julio ametoa pendekezo la mchezaji huyo kwa sababu anataka kuungana naye tena kwani walishawahi kufanya kazi pamoja wakati akiifundisha Namungo.
Wakati KMC ikihitaji saini ya Kikoti, tayari imewasajili Juma Shemvuni aliyekuwa anaichezea Mbeya City iliyoshuka daraja, Muhsin Malima (Dodoma Jiji) na Rodgers Gabriel aliyetoka Pamba FC.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live