Dakika 45 za kipindi cha kwanza zinakamilika katika Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam sio wenyeji Yanga wala wageni Al Hilal kutoka kule nchini Sudan waliofanikiwa kupata goli.
Mchezo huo wa mkondo wa kwanza kuwania kufuzu kwa hatua ya makundi Ligi ya Mabingwa Afrika umewashuhudia Yanga wakiwa bora katika kuutawala mchezo licha ya kutopata bao.
Yanga wamefanikiwa kufanya masha,mbulizi kadhaa ya hatari langoni mwa Al Hilal huku Aziz Ki na Fiston Mayele wakipoteza nafasi kadhaa.
Winga Bernard Morisson ameonekana kuipa tabu safu ya ulinzi ya Al- Hilal huku akitengeneza nafasi kadhaa.
Prngine kila timu inakwenda kufanya mabadiliko ya mbinu ili kuweza kupata matokeo katika mchezo wa leo.