Sat, 11 Feb 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Dakika 45 za Kipindi cha kwanza zinakamilika katika Uwanja wa Jenerali Lansana Conte, mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika hatua ya Makundi.
Wenyeji Horoya wanakwenda mapumziko wakiwa kifua mbele kwa uongozi wa bao 1-0 lililowekwa wavuni na P. Ndiaye dakika ya 18 ya mchezo akiunganisha mpira wa kona.
Ni muda wa mwalimu Robertinho kutazama mapungufu ya kikosi chake na kufanya mabadiliko katika maeneo yaliyosababisha washindwe kutimiza lengo katika dakika 45 za kipindi cha kwanza.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live