Mchezaji wa klabu ya Manchester City na timu ya taifa Ubelgiji, Kevin De Bruyne amesema kwamba hakuhudhuria sherehe za utoaji wa tuzo za Ballon D'Or kwasababu hizo si tuzo za haki bali ni za rushwa
"Hii tuzo ni kama vile Utani sio kitu cha kweli, haiwezekani Mshindi wa Tuzo atangazwe wiki moja nyuma kabla ya kutolewa tuzo. Kama tuzo hii ingekuwa Fair pasinamashaka Haaland angeshinda tuzo kwasababu alistahili kuwa mshindi kwakua alifanya kila kitu ambacho mshindi anapaswa kuwanacho.
Kwahiyo sikuhudhuria katika tuzo kwasababu sipendi kuwa sehemu ya Rushwa" amesema KDB
Mwaka huu nchini Ufaransa ndipo zilipofanyika utoaji wa tuzo hizo na Dunia nzima ilimshuhudia Lionel Messi akitwaa tuzo yake ya 8 na kuandika Historia ya kuwa mchezaji pekee mwenye Ballon D'or nyingi duniani.