Mtangazaji wa Wasafi fm na ICU ya Maisha magic Bongo, Juma Lokole ametangaza rasmi kuacha kuishabikia timu ya yanga na kuhamia timu ya Azam akidai kwamba amekuwa akimshabia sana Feisal Salum na hawezi kumuacha popote atakapoenda atamfuata.
Lokole ambaye awali alikuwa Shabiki wa timu ya Simba aliamua kuihama timu hiyo baada ya Haji Manara kuhamia Yanga ambapo alisema kwamba anamkubali sana Manara ndiyo maana aliamua kumfuata Yanga.
Lokole ameendeleza tabia hiyo ya kudonyoadonyoa ushabiki ambapo jana ametangaza kuwa yeye siyo Shabiki wa Yanga tena, kwa sasa ameamua kuweka mapenzi yake ya kiushabiki katika Klabu ya Azam huku sababu kubwa ikiwa ni kumfuata Feisal Salum.