Wed, 14 Aug 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kiungo wa Real Madrid, Jude Bellingham anatumiwa na kikosi hicho kumshawishi rafiki yake mlinzi wa Liverpool, Trent Alexander-Arnold ajiunge na wababe hao wa Hispania.
Jude na Arnold ni marafiki wa karibu zaidi kutokana na wote kuichezea timu ya taifa Uingereza na Madrid wanataka kutumia mwanya huo kumnasa Arnold.
Klabu ya FC Barcelona nayo inamfuatilia kwa ukaribu mlinzi huyo wa pembeni ambaye mkataba wake unatarajiwa kumalizika Mwaka 2025.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live