Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Jose Mourinho anukia Cameroon

Jose Mourinho Portugal.jpeg Jose Mourinho

Tue, 26 Mar 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Majadiliano kati ya Kocha kutoka nchini Ureno Jose Mourinho na Shirikisho la Soka nchini Cameroon ‘FECAFOOT’ yanaonekana kupiga hatua kubwa kwa ajili ya kocha huyo kuinoa ‘The Indomitable Lion’.

Cameroon imekuwa katika mchakato wa kumsaka Kocha Mkuu wa Mpya wa Kikosi chao cha Taifa, baada ya kuachana na Kocha mzawa Rigobert Song mwezi uliopita.

José Mourinho anatafuta changamoto mpya baada ya kuachana na klabu ya AS Roma ya Italia Januari 2024, kufuatia mfululizo mbaya wa matokeo ligi kuu Italia.

‘The Special One’ anaweza kuchukua mikoba ya kuinoa timu ya taifa ya Cameroon endapo mazungumzo yatakwenda vizuri na Cameroon.

Ingawa Mourinho anapewa nafasi kubwa ya kuwa kocha mkuu wa timu ya taifa mshahara unaweza kuwa kikwazo kati yake na Cameroon.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live