Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Job amuomba radhi Kocha Taifa Stars

Job X Morocco Job amuomba radhi Kocha Taifa Stars

Wed, 19 Jun 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Beki wa kati wa Klabu ya Yanga, Dickson Job amemuomba Radhi Kocha wa Taifa Stars Ahmed Morroco Kufuatia Kutoelewana Kwao Jambo lililopelekea Dickson Job kutoitwa Katika Kikosi cha Stars Kinacho wania Kufuzu Kombe la Dunia 2026.

Dickson Job amekuwa na Mgogoro na Kaimu kocha Mkuu wa taifa Stars Ahmed Morroco Akihusishwa na Kugomea Kucheza Katika Michuano ya Afcon2023 (Ivory Coast) pia Ikisemwa Dickson Job alipewa Majukumu na Mwalimu wake huyo Kucheza Namba Fulani na Kisha yeye akakataa.

Dickson Job Kupitia Kipindi cha #KipengaExtra cha East Africa Redio na East Africa TV kwa Mara ya Kwanza Dickson Job anakanusha Madai hayo yaliyopelekea Mpaka Kuonekana sio Mzalendo wa taifa lake.

Dickson Job anasema yeye hajawahi Kugomea Majukumu aliyopewa na Mwalimu huyo na Kuhusishwa na Kugomea Taifa Lake Jambo ambalo sio Kweli.

Yote kwa yote Dickson Job ametumia Nafasi hiyo Kumuomba Radhi Mwalimu wake Ahmed Morroco na Kuwaomba Radhi Watanzania ambao walikwazika kwa namna moja hama Nyingine Baada ya Kusikia Uvumi wa Kutokuwa Mzalendo Juu ya Taifa lake.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live