Mon, 20 Dec 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Hakika, juhudi zinaweza kukupa mchongo. Joao Cancelo ni mfano tosha katika hili. Juhudi zake zinamfungulia milango mikubwa pale Etihad.
Cancelo amekuwa kwenye kiwango bora msimu huu ndani ya kikosi cha Pep Guardiola. Akicheza kama beki wa kulia, huwezi kusema Cancelo ni beki hasa, mchango wake kwenye mashambulizi na mfumo wa uchezaji wa Man City, ni mkubwa kadiri siku zinavyozidi kwenda.
Japokuwa Joao Cancelo bado anamkataba na City mpaka 2025, imeripotiwa klabu hiyo ipo mbioni kuboresha zaidi mkataba wake ikiwa ni pamoja na kumuongezea mshahara wa takribani Pauni 100,000.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live