Sun, 14 May 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kocha mkuu wa Yanga Professor Mohamed Nasreddine Nabi ameonesha nia ya kuinasa saini ya beki wa Marrumo Gallants kuelekea msimu ujao.
Bado hakuna mazungumzo yoyote baina ya Yanga na mchezaji Mpho Mvelase hadi sasa.
Taarifa Kutoka ndani ya Uongozi wa Yanga unatarajiwa kukutana na wakala wa Mpho Mvelase nchini Afrika ya kusini siku ya jumanne kuanza mazungumzo.
Pia baadhi ya vyombo vya habari nchini Afrika ya kusini vishaanza kuripoti taarifa hii ya beki Mpho Mvelase kutakiwa na Mabingwa wa Tanzania Yanga SC.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live