Mon, 18 Dec 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Jina la Kiungo Mshambuliaji wa Wealdstone FC ya Uingereza, Tarryn Allarakhia (26) limejumuishwa rasmikwenye kikosi cha Taifa Stars kitacho kwenda kwenye Mashindano ya AFCON 2024 nchini Cameroon.
Kwa mujibu wa Menejimenti inayomsimamia Tarryn imeeleza kwamba jina la mchezaji huyo ni miongoni mwa majina 55 ya mwanzo ambayo TFF Kupitia kwa Kocha wa Taifa Stars wameyapokea tayari kwa mchujo kuelekea AFCON.
Pia, Kocha huyo amemjumuisha beki wa kati ambaye pia anaweza kucheza kama beki wa kulia na beki wa kushoto, Roberto Nditi, 23 anayekipiga Forfar Athletic FC, ya Scotland, United Kingdom.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live