Kocha na mchezaji mkongwe wa Simba, Jamhuri Kihwelo Julio amesema kwa msimu huu mshambuliaji wa Yanga, Fiston Mayele amefanya kazi nzuri n ani straika halisi kwa kuwa anajua kufunga.
Amesema “Licha ya kuwa mpira wa sasa hivi combination imesababisha wachezaji wengi kufunga magoli lakini Mayele anaweza kufunga popote.
“Tabu anayopata kwa sasa ni kuwa anakabwa sana, kwanza mastraika wengi siyo mafundi wa kumiliki mpira lakini Mayele ni fundi, anaweza kuukontroo mpira na kuuchezea, anaweza kupiga cheka na kutoa pasi.
“Angalia kama goli alilofunga juzi, straika mwingine ni ngumu kufunga, anatumia miguu yote miwili.