Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Jesse Lingard kutimkia Saudi Arabia

Jesse Lingard Looks On During Nottingham Forest Pre Season Friendly Against Valencia Jesse Lingard

Wed, 18 Oct 2023 Chanzo: Dar24

Mchezaji wa zamani wa Manchester United, Jesse Lingard anakaribia kusaini katika klabu ya Saudia Pro League, AI Ettifaq mara baada ya muda wake wa kutazamwa mwenendo wake kwenda vizuri.

Klabu hiyo inanolewa na nahodha wa zamani wa England na Liverpool, Steven Gerrard imeweka wazi kuwa msimu ujao watakuwa na Lingard baada ya kuridhishwa na maendeleo yake.

Gerrard anataka kumsajili Lingard lakini itabidi asubiri hadi mwezi Januari kutokana na sheria za kusajili wachezaji wa kigeni nchini Saudi Arabia kubana kwa sasa.

Wachezaji wa kigeni Saudi wanapaswa wasizidi 8 kwenye orodha wa wachezaji wanaocheza mechi na mpaka sasa Al Etifaq ina wachezaji 10 wa kigeni.

Kwa mantiki hiyo kuna namna ambavyo klabu hiyo itawatoa baadhi ya wachezaji ili wapitishe jina la Lingard.

Chanzo: Dar24