Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA) kupitia Kamati yake ya Utendaji kimemteua Jemedari Said Kazumari maarufu kama Bin Kazumari kuwa Mwenyekiti wake kwenye Kamati ya tuzo za Mwanamichezo bora.
Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA) kupitia Kamati yake ya Utendaji kimemteua Jemedari Said Kazumari maarufu kama Bin Kazumari kuwa Mwenyekiti wake kwenye Kamati ya tuzo za Mwanamichezo bora. Tuzo za Mwanamichezo bora wa TASWA hutolewa kila mwisho wa mwezi kwa Mwanamichezo aliyefanya vizuri kwa mwezi husika na mwisho wa mwaka hutunuku pia wanamichezo bora wa mwaka.