Wakati taarifa zikiendelea kusambaa kuwa sababu ya Mlinzi wa Yanga Dickson Job kutoitwa katika kikosi cha Timu ya Taifa ni kutokana na kitendo chake cha kugoma kucheza katika mechi dhidi ya Dr Congo.
Mchambuzi wa Michezo kutoka Efm, Jemedari Said amesema ili kumsaidia mchezaji huyo na kutambua ubaya wa kile alichokifanya;
Kupitia Kurasa zake za mitandao ya Kijamii, Jemedari ameandika;
Kumsaidia Dickson Job ni kumueleza pale alipokosea na sio kumtetea kwenye makosa ya wazi. Kumueleza mtu makosa yake haimaanishi humpendi kama wengi wanavyodhani ila unamuweka kwenye njia sahihi. Kukataa kucheza mechi ya timu ya Taifa tena kwenye mashindano na upo camp ni usaliti.