Sun, 30 Jul 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kiungo wa zamani wa Real Madrid, James Rodriguez amejiunga na klabu ya São Paulo ya Ligi kuu Brazil kwa uhamisho huru akitokea Olympiacos.
James (32) raia wa Colombia amesaini mkataba wa miaka miwili.
James ambaye aling'ara sana kwenye kombe la Dunia 2014, amechezea klabu 10 tofauti katika mataifa 10 tofauti.
Envigado, Banfield, FC Porto, AS Monaco, Real Madrid, Bayern Munich, Everton, Al-Rayyan, Olympiacos na sasa São Paulo.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live