Mon, 27 May 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Wasiwasi wa James Akaminko kuondoka ndani ya Azam FC umeongezeka baada ya hapo jana Azam FC kukamilisha usajili wa kiungo Ever Meza kutokea Leonnes ya nchini Colombia.
Za ndani kabisa zinadai kuwa nyota huyo ampema alishaomba kwenda kutafuta changamoto mpya sehemu nyingine na inawezekana Ever Meza ndiye anaekwenda kuchukua nafasi ya Akaminko.
Simba SC imekuwa ikitajwa mara kadhaa kuiwinda saini ya kiungo huyo raia wa Ghana ambae amekuwa kwenye kiwango Bora sana akiwa na Azam FC.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live