Mwanamitandao Jake Paul (27) atazichapa na Mike Tyson mnamo Julai 20, 2024 katika uwanja mkubwa wa AT&T, imethibitishwa. Pambano hilo litarushwa LIVE kupitia Netflix ambao ndio waandaaji wakishirikiana na Kampuni ya Most Valuable Promotions.
Mwanamitandao Jake Paul (27) atazichapa na Mike Tyson mnamo Julai 20, 2024 katika uwanja mkubwa wa AT&T, imethibitishwa. Pambano hilo litarushwa LIVE kupitia Netflix ambao ndio waandaaji wakishirikiana na Kampuni ya Most Valuable Promotions. Tyson (57) ambaye ni bondia wa zamani wa uzito wa juu, mara ya mwisho kupanda ulingoni ilikuwa ni mwaka 2020 kwenye pambano la maonesho dhidi ya Roy Jones Jr, pambalo ambalo lilimalizika kwa sare.