Thu, 14 Dec 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Timu ya JKT Tanzania imefanikiwa kutinga Hatua ya 32 Bora michuano ya Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), maarufu kama Azam Sports Federation Cup (ASFC) baada ya ushindi wa 5-0 dhidi ya Kurugenzi ya Simiyu.
Mabao ya JKT Tanzania yamefungwa na Mohamed Bakari dakika ya 60, Ismail Aziz Kader dakika ya 65, Edward Songo dakika ya 15 kwa penalti, 89 na 90 na ushei.
Mechi nyingine za Hatua ya 64 Bora leo ASFC Ihefu SC imeitoa Rospa FC ya Mtwara kwa kuichapa mabao 3-0 Uwanja wa Highland Estate, Mbarali mkoani Mbeya, Coastal UniĆ³n imeichapa Greenland ya Kagera mabao 2-0.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live