Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

JKT Tanzania yavuta kifaa kutoka Zenji

JKT TZ ZNZ JKT Tanzania yavuta kifaa kutoka Zenji

Fri, 29 Dec 2023 Chanzo: Dar24

JKT Tanzania inaendelea kuimarisha kikosi kwenye usa jili wa dirisha dogo na tayari imemalizana na straika wa IKU ya Zanzibar, Gamba ldd Matiko anayemiliki mabao sita katika Ligi Kuu Zanzibar (ZPL).

Ingawa haijajulikana kasaini mkataba wa muda gani, Matiko atajiunga na JKT Tanzania muda wowote.

Mchezaji huyo ambaye ni kinara wa mabao JKU inayoongoza ZPL kwa ponti 36 ikiwa imefung mabao 21.

Gamba ldd alianza kufuatiliwa na JKT Tànzania baada ya kuifunga Singida Fountain Gate katika Kombe la Shirikisho Arika.

Mmoja wa viongozi wa timu hiyo alisema kupitia usajili unaoendelea wataongeza wachezaji wanne, lakini pia wapo ambao watakatwa kwa kutoonyesha ubora.

Ukiondoa Kichuya ambaye tayari kasaini, alisema kuna Matiko na wengine wawili ambao bado wanazungumza nao na mambo yakiwa tayari watajiunga na timu.

Chanzo: Dar24