Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

JKT Tanzania yasogea nafasi ya tano

TFFD.png JKT Tanzania yasogea nafasi ya tano

Mon, 14 Mar 2022 Chanzo: www.mwanaspoti.co.tz

JKT Tanzania imepanda  nafasi ya tano kutoka  ya saba, kwenye msimamo wa Ligi ya Championship, baada ya kuitandika Pan African kwa mabao 2-1, mchezo uliopigwa Uwanja wa Uhuru Dar es Salaam.

Baada ya ushindi huo, JKT Tanzania imevuna alama 32, ikiishusha KenGold kutoka nafasi ya tano hadi ya sita kwa utofauti wa mabao.

Mchezo huo ulikuwa na ushindani mkali, Pan African licha ya kuchapwa mabao 2-1, walinzi wake walikuwa imara kupunguza presha ya washambuliaji wa JKT Tanzania waliokuwa wanafika mara kwa mara golini kwao, kipindi cha pili cha mchezo huo.

Kipindi cha Kwanza, Pan African ilitawala mchezo na ilikosakosa mabao, jambo lililowagharimu kipindi cha pili  baada ya JKT Tanzania kurejea na mbinu ya kushambulia zaidi iliyowapa matunda ya ushindi.

Mchezaji wa JKT Tanzania Ibrahim Mohamed, amesema haukuwa mchezo rahisi jambo  muhimu kwao ni pointi tatu.

"Pointi tatu kwanza mengine baadae, ligi imefika pagumu kila timu ina mahesabu makali ya kupanda Ligi Kuu Bara."amesema.

Chanzo: www.mwanaspoti.co.tz