Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Ivory Coast, Afrika Kusini zatinga Nusu Fainali AFCON

B24mcwm3073 Ivory Coast, Afrika Kusini zatinga Nusu Fainali AFCON

Sun, 4 Feb 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

WENYEJI, Ivory Coast wamefanikiwa kutinga Nusu Fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika baada ya ushindi wa 2-1 dhidi ya Mali katika mchezo uliodumu kwa dakika 120 usiku wa jana Uwanja wa Bouaké mjini Bouaké.

Kiungo wa Red Bull Salzburg ya Ausrtia, Nene Dorgeles alianza kuifungia Mali dakika ya 71, lakini mshambuliaji wa Brighton & Hove Albion ya England, Simon Adingra akaisawazishia Ivory Coast dakika ya 90.

Baada ya sare ya 1-1 ndani ya dakika 90, mchezo huo ukaenda kwenye dakika 30 nyongeza, ambako mshambulaji wa Reims ya Ufaransa, Oumar Diakité aliwafungia wenyeji bao la ushindi dakika ya 120.

Katika mchezo mwingine wa Nusu Fainali jana, Afrika Kusini iliitoa Cape Verde kwa penalti 2-1 kufuatia sare ya bila kufungaa ndani ya dakika 120, huku Ronwen Hayden Williams akiweka rekodi ya kuwa kipa wa kwanza kuokoa penalti nne katika AFCON Kihistoria.

Kipa huyo wa Mamelodi Sundwons, aliokoa penalti za Bebé, Willy Semedo, Laros Duarte, Patrick Andrade huku ya Bryan Teixeira pekee ndiyeo ilimpita na kutinga nyavuni.

Waliofunga pennalti za Bafana Bafana ni Teboho Mokoena na Mothobi Mvala, huku Zakhele Lepasa na Aubrey Modiba wakikosa pia upande wa Afrika Kusini.

Sasa Afrika Kusini itakutana na Nigeria, wakati Ivory Coast itacheza na DRC katika Nusu Fainali ambazo zitapigwa Jumatano.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live