Thu, 18 Jul 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Winga wa Yanga, Skudu Makudubela alisaini mkataba wa miaka miwili na Yanga huku akiahidiwa kupewa pesa ya usajili sign-on-fee ya $45,000 (Tsh 117,000,000) na wakati anasaini Yanga walimlipa $25,000 huku $20,000 iliyobaki akiahidiwa kupewa mwanzoni mwa msimu wa 2024/25.
Hivyo kama Yanga wanataka kuachana na mchezaji huyo kwenye dirisha hili la usajili wanatakiwa kuvunja mkataba wake kwa kumlipa $20,000, iliyobaki Na mshahara wa msimu mzima ambao angepokea 2024/25.
Ikumbukwe Skudu analipwa $6000 (Tsh 15,930,000) kila mwezi hivyo mshahara wake wa mwaka Mzima ni $72,000 (Tsh 191,160,000).
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: