Thu, 19 Oct 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kocha Mkuu wa Simba SC, Roberto Oliviera 'Robertinho' amesema kwa mtazamo wake, Henock Inonga ndiye beki bora wa kati kwa sasa Afrika.
Robertinho ameyasema hayo alipkuwa kwenye mkutano wa waandishi wa habari kuelekea mchezo wao wa kesho dhidi ya Al Ahly utakaopigwa kwenye Uwanja wa Benjamini Mkapa jijini Dar.
“Kwa mtazamo wangu Inonga ndio beki bora zaidi wa kati Afrika, natarajia kumtumia kwenye mechi dhidi ya Al Ahly kesho, uzuri wake ana uwezo wa kukaa na mpira na anajiamini hivyo ni muhimu aanze kesho ili mbinu ikamilike,” alisema Robertinho.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live