Mon, 26 Feb 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba SC, Ahmed Ally, amesema mgeni rasmi kwenye mchezo wao dhidi ya Jwaneng Galaxy atakuwa ni beki wao wa kati, Henock Inonga.
Ahmed ameyasema hayo leo alipokuwa akielezea maandalizi ya mchezo huo utakaopigwa Jumamosi kwenye Uwanja wa Benjamini Mkapa jijini Dar.
“Mgeni rasmi katika mchezo dhidi ya Jwaneng Galaxy ni Henock Inonga sababu ndio mchezaji pekee katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kati ameifikisha timu yake ya taifa kwenye nafasi ya nne kwenye AFCON 2023.”- Ahmed Ally. #WenyeNchi
Chanzo: www.tanzaniaweb.live