Thu, 15 Sep 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Beki wa kati wa klabu ya @simbasctanzania na raia wa DR Congo @inonga_baka_varane ameitwa kwenye kikosi cha timu ya taifa ya Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
Inonga amekuwa mchezaji pekee kutoka ligi kuu ya Tanzania bara NBC kuitwa kwenye kikosi cha timu ya taifa.
Ikumbukwe kuwa ligi kuu ya Tanzania bara ina wachezaji wengi sana kutoka nchini Congo wakiwemo wachezaji kadhaa wa Yanga kama Mayele, Bangala, Djuma Shabani na wengine.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live