Tue, 9 Apr 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Beki kisiki wa Simba SC, Henock Inonga, hatakuwa sehemu ya mchezo wa leo dhidi ya Mashujaa FC katika mchezo wa CRDB FA.
Kocha msaidizi, Selemani Matola, amesema wachezaji wote waliosafiri na timu kutokea Misri kucheza na Al Ahly wako fiti isipokuwa Inonga ambaye alipata maumivu ya goti.
"Wachezaji wote wapo fiti isipokuwa Inonga ambaye alipata majeraha ya goti, hatukupata muda wa kutosha kupumzika lakini tuliijua hii ratiba kabla ya kwenda hivyo tumejipanga kupata matokeo," alisema Matola.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live