Kuelekea mchezo wetu ujao dhidi ya Dodoma Jiji FC, tutawakosa wachezaji wawili [Henock Inonga na Aubin Kramo] ambao wanachangamoto kidogo za majeraha.
Inonga alipata changamoto kwenye mchezo wa Nusu Fainali ya Ngao ya Jamii dhidi ya Singida Fountain Gate FC ambapo alianguka dakika ya 89 na kuumia bega baada ya pale alishindwa kuendelea na mchezo kutokana na maumivu makali akatolewa nje.
Ameshamaliza awamu ya pili ya matibabu na leo tunatarajia ataanza mazoezi ya pamoja na wenzake [group training] na tutaangalia kama atakuwa tayari kuingia kwenye machaguo ya mwalimu. Hiyo yote itategemea na namna ambavyo ataweza kufanya mazoezi.
Dkt. Edwin Kagabo, daktari wa Simba.