Tue, 9 Jan 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Rais wa Yanga SC, Injinia Hersi Said, amesema hana sababu ya kulalamika kuhusu kutoshiriki Kombe la Afican Football League (AFL) lilipoanzishwa mwaka jana lakini alichohakikishiwa ni kwamba, mwaka huu wanashiriki.
Injinia amesema amezungumza ma Rais wa CAF, Patrice Motsepe, amemhakikishia kwamba watashiriki mwaka huu na kwamba msimu uliopita kulikuwa na idadi chache ya timu zilizotakiwa.
"Alinieleza kwamba kulikuwa na limited number ya klabu zilizohitajika na hatuna budi kuheshimu kauli za viongozi, muhimu kwa kauli yake ametuhakikishia kwamba mwaka huu tutashiriki," alisema Injinia.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live