Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Infantino: Tuwalinde wachezaji

Mastaa Simba Wajiachia Na Infantino X Wenger.jpeg Infantino: Tuwalinde wachezaji

Wed, 13 Dec 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Rais wa Fifa Gianni Infantino amesema tukio la Rais wa Ankaragucu Farukhilo Rais wa Ankaragucu Faruk mwamuzi Halil Umut Meler na vurugu "hazina nafasi katika mchezo wetu, "Bila wasimamizi wa mechi hakuna soka," alisema.

“Waamuzi, wachezaji, mashabiki na wafanyakazi wanatakiwa kuwa salama ili kufurahia mchezo, na nitoe wito kwa mamlaka husika kuhakikisha hili linatekelezwa kikamilifu na kuheshimiwa katika ngazi zote.

Rais wa Ankaragucu Faruk Koca akamatwa baada ya kumshambulia mwamuzi, Waziri wa Sheria Yilmaz Tunc alisema Koca na wengine wawili walikamatwa rasmi kwa "kumjeruhi afisa wa umma".

Timu ya Rais wa Ankaragucu Faruk Koca ilikubali bao la kusawazisha dakika ya 97 katika sare ya 1-1 na Caykur Rizespor, Wenyeji Ankaragucu walikuwa wametangulia mapema katika mechi ya Super Lig Jumatatu usiku kabla ya mchezaji wao kutolewa kwa kadi nyekundu baada ya dakika 50. Caykur alisawazisha dakika za mwisho baada ya mchezaji pia kutolewa kwa kadi nyekundu, na matukio ya fujo yakafuatia baada ya kipenga cha mwisho.

Mehmet Yorubulut, daktari mkuu wa hospitali ya Acibadem, alisema Meler hajapata madhara yoyote ya ubongo na kuna uwezekano akaruhusiwa kuruhusiwa siku ya Jumatano.

"Kuvuja damu kwenye jicho la kushoto la Meler kulianza kupungua," alisema Yorubulut, ambaye aliongeza hakutakuwa na madhara ya kudumu.

Meler, ni mmoja wa waamuzi wakuu wa Uturuki na anasimamia michezo ya kimataifa ya Fifa.

Pia yumo kwenye orodha ya waamuzi wakubwa wa Uefa na alichezesha mechi ya nusu fainali ya Ligi ya Europa Conference ya West Ham dhidi ya AZ Alkmaar msimu uliopita na akasimamia mchezo wa kundi la Lazio wa Ligi ya Mabingwa dhidi ya Celtic mwezi uliopita.

Kulingana na mashirika ya habari ya Uturuki, Meler alisema: "Faruk Koca alinipiga ngumi chini ya jicho langu la kushoto nilianguka chini. Nilipokuwa chini, watu wengine walinipiga teke usoni na sehemu nyingine za mwili wangu mara nyingi."

Chanzo: www.tanzaniaweb.live