Ni balaa ndivyo unavyoweza kusema kwa jinsi mashabiki walivyojitokeza kwa wingi kwenye Uwanja wa Ilulu kutazama mchezo kati ya Namungo na Yanga.
Yanga Iko ugenini mkoani Lindi kuikabili Namungo katika mchezo utakaoanza saa 10:00 jioni.
Hadi kufikia saa 6:00 mchana sehemu kubwa ya Uwanja umejaa huku nje bado kukiwa na idadi kubwa ya watu.
Mageti ya uwanjani yalifunguliwa kuanzia Saa 4:30 asubuhi na mashabiki kuanzia kuingia uwanjani lakini hadi kufikia saa sita mchana Uwanja umefurika huku mashabiki wakiendelea kuingia.
Licha ya kwamba mechi inaanzia Saa 10 jioni lakini mashabiki hawajali kwamba watakaa muda mrefu kusubiri mchezo huo huku wale wa mzunguko wakipata tabu zaidi kwani jukwaa lao hakuna mahali pa kukaa Bali ni mwendo wa kusimama hadi mpira unaisha.