Mon, 4 Dec 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Sare ya 0-0 leo kwenye mchezo wa raundi ya 13 kati ya Prisona dhidi ya Ihefu imeifanya ihefu kufikisha siku 60 bila kuonja ushinda kwenye mechi 8 mfululizo tangu iliipoichapa Yanga Octoba 4 mabao 2-1 katika Uwanja wa Highland Estate, Mbeya.
Ihefu imekuwa haina mwendelezo mzuri baada ya kupata sare nne sawa na idadi ya mechi walizopoteza huku Kocha Basena akiwa amesimamia mechi saba tu tangu alipojiunga na timu hiyo Octoba 16.
Prisons amabayo ipo nafasi ya 13 ikiachana nafasi moja na Ihefu, imeshinda mechi mbili, kutoka sare tano, kupoteza mechi tano na inapointi 11 katika mechi 12.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live