Mon, 19 Feb 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Upepo umeendelea kuwa mzuri kwa Ihefu FC, wameendelea kushusha kipigo na safari hii, wamewachapa Geita Gold.
Geita waliokuwa nyumbani katika uwanja wa Nyamkumbu, wamelazimika kupokea kipigo hicho kilichotekelezwa barabara na Elvis Rupia na Marouf Tchakei.
Goli pekee la kufutia machozi liliwekwa kambani na Tariq Seif. Hii ni mechi ya pili mfululizo Ihefu anashinda ugenini, kabla ya hiyo, alimchapa Mtibwa 3-2.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live