Wed, 6 Dec 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Ihefu FC yenye maskani yake Mbarali mkoani Mbeya imefikia makubaliano ya kuvunja mkataba na kocha Mganda, Moses Basena.
Basena amedumu katika kikosi hicho kwa siku 50 tangu alipotambulishwa Oktoba 16 huku akikumbana na matokeo ya sare na kufungwa bila kupata ushindi katika mechi saba.
Basena alichukua mikoba ya kocha Zuberi Katwila.
MECHI ALIZOONGOZA BASENA
Ihefu 0-0 Coastal Union
Simba 2-1 Ihefu
Singida FG 2-2 Ihefu
Ihefu 1-3 Azam FC
Namungo 2-0 Ihefu
JKT Tanzania 1-1 Ihefu
Ihefu 0-0 Prisons.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live