Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Huyu hapa Pilato mechi ya Azam vs APR

Eswatini Mwamuzi kutoka Eswatini, Thulani Sabelo Sibandze

Fri, 16 Aug 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Mwamuzi kutoka Eswatini, Thulani Sabelo Sibandze ndiye atakayesimamia mchezo wa hatua ya awali kati ya Azam FC na APR FC katika mashindano ya klabu bingwa Afrika.

Mtanange huo utapigwa katika uwanja wa Azam Complex Chamanzi Agosti 18 majira ya saa kumi na mbili kamili za jioni.

APR FC ndio Mabingwa wa Ligi Kuu nchini Rwanda msimu uliopita ambapo pia walikipiga na Simba SC kwenye “Simba Day” katika kupima kikosi kuelekea Ligi Kuu na Mashindano ya Kimataifa.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live