Mshambuliaji wa Klabu ya Al Nassr ya Saudi Arabia, Clara Luvanga ametoa kauli inayooneka kuwashangaza wengi baada ya kusema kuwa Rais wa Klabu ya Yanga Injinia Hersi Said alimruhusu bure kujiunga na Klabu ya nchini Hispania Licha ya kuwa alikuwa na Mkataba wa Miaka miwili na Yanga.
Akizungumza Clara anasema;
"Timu kutoka Spain ilinifuata ikitaka huduma yangu na hapo nilikuwa tayari nimeshasaini mkataba mpya na Yanga wa Miaka miwili kwahiyo nikamfuata Eng. Hersi kumshirikisha hilo jambo na yeye akaniambia haina shida nenda, hatutokulipisha chochote na kama ukifanikiwa basi uje kutusalimu."
"Aliniambia anapenda sana wachezaji wa kike wakifanikiwa kucheza soka kimataifa na ndio maana hakusita kuniacha niende."
Maneno ya Mshambuliaji wa Twiga Stars na Klabu ya Al Nasri, Clara Luvanga