Mchambuzi na Mtangazaji wa michezo Shafii Dauda, amesema Simba hawaangalii mwisho wa msimau utakuwaje, wanachoangalia ni ushindi katika kila mechi yao.
Shafii amesema, endapo mechi ya Jumapili hii ya dabi Simba akishinda, atazidi kujiongezea kujiamini zaidi.
“Mpaka sasa hivi Simba kashinda mechi zote kwa 100% kwa hiyo akimfunga Yanga ambaye ndio mpinzani wake namba moja ataweka gap lakini pia ataongeza confidence, hiyo itakuwa zaidi ya matokeo na itaenda kubadilisha kila kitu.”
“Simba na Yanga anayewahi kutengeneza saikolojia ndiye anayewini, nimeangalia mechi zao zote hawajali mwisho wa msimu itakuwaje wao wanadili na mechi iliyo mbele yao na sasa anayefuata ni Yanga”