Wed, 7 Feb 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Chama cha Soka Misri (EFA) kimemtangaza Mfungaji bora wa muda wote wa timu ya Taifa ya Misri, Hossam Hassan kuwa kocha mkuu mpya wa timu ya taifa ya nchi hiyo.
Hossam anachukua mikoba ya Mreno, Rui Vitoria aliyefutwa kazi hivi karibuni kutokana na mwenendo usioridhisha wa Mafarao hao kwenye fainali za mataifa ya Afrika (AFCON) zinazoendelea Nchini lvory Coast.
Hossam (57) ambaye amewahi kuvitumikia vilabu vya Al Ahly na Zamalek aliichezea Timu ya Taifa Misri mechi 178 huku akifunga mabao 69.
Katika majukumu hayo ya kuinoa Misri, Hossam Hassan atasaidiwa na pacha wake, Ibrahim Hassan.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live