Fri, 23 Feb 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mshambuliaji nyota wa Manchester United, Rasmus Hojlund (21) anatarajiwa kuwa nje ya uwanja kwa wiki tatu kutokana na majeraha.
Nyota huyo aliyeko katika kiwango bora hivi sasa amepata jeraha la misuli na atakosa michezo kadhaa ya timu hiyo.
Kupata majeraha kwa Hojlund kunaongeza majeruhi katika chumba cha majeraha cha United na kuungana na majeruhi wengine ambao ni Luke Shaw, Mason Mount, Lisandro Martinez.
Majeraha hayo ya Hojlund yatamfanya akose michezo mitatu ya Fulham, Nottigham Forest na Manchester City.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live